Utambulisho katika Kristo: Wewe ni Nani Machoni pa Mungu? - Mwongozo #1
- Pr Enos Mwakalindile
- 23 hours ago
- 1 min read
Utambulisho katika Kristo ni mwaliko wa kuacha majina ya zamani ya aibu, hukumu, na kushindwa, na kusikia kwa upya kile Mungu anachosema juu ya maisha yako ndani ya Yesu. Somo hili linatukumbusha kwamba wewe si makosa yako, si sauti za watu, wala si maumivu ya jana yako, bali ni mtu aliyeumbwa, aliyeitwa, aliyependwa, na anayefanywa mpya katika Kristo. Hivyo, kwa kuamini Injili na kuruhusu Neno la Mungu litawale kuliko sauti za lawama, tunaanza kutembea katika uhuru wa kweli kama watoto wa Mungu.

Kwa Tafakari Zaidi Sikiliza Nyimbo:
Kwa Maarifa Zaidi Soma Makala:
· Umechaguliwa na Mungu: Siri ya Upendo Ulio Tangulia Mwanzo wa Dunia
· Msalaba: Upatanisho na Haki ya Mungu
Somo Lijalo: Msamaha na Toba – Uhuru Kutoka kwa Hatia na Aibu.




Comments