Uchambuzi wa 2 Wafalme 1 — Moto Mlimani, Unabii wa Kitandani cha Ugonjwa, na Mungu Asiyekubali Kushauriwa Kama Sanamu
- Pr Enos Mwakalindile
- Feb 24
- 1 min read
Mfalme anaanguka.
Siyo vitani—bali kutoka juu ya dirisha la roshani.
Siyo kwa mkuki wa adui—bali kwa kujikwaa kwake mwenyewe.
Na baada ya kishindo, kunapokaa kimya,
anaanza kumtafuta mungu anayemudu kumdhibiti.
Mungu wa kushauriwa bila toba.
Mungu asiyeuliza habari za mashamba ya mizabibu.
Lakini Mungu aliye hai si laini ya dharura.
Si hirizi.
Si sanamu yenye huduma kwa wateja.
Ndipo nabii anasimama njiani,
na swali linatua kama radi:
“Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli?”
Hii ni 2 Wafalme 1.

Ikawa, baada ya kufa kwake Ahabu, Moabu wakawaasi Israeli. 2 Na Ahazia akaanguka katika dirisha la chumba chake orofani, katika Samaria, akaugua; akatuma wajumbe, akawaambia, Enendeni mkaulize kwa Baal-zebubu, mungu wa Ekroni, kwamba nitapona ugonjwa huu....




Very insightful read