Uchambuzi wa 2 Wafalme 24 — Mto Unapopungua Maji, na Uhamisho wa Awamu Unapoanza
- Pr Enos Mwakalindile
- 11 hours ago
- 1 min read
Mageuzi yameisha. Mfalme amezikwa. Na historia inashika kasi.
Mbingu zinakuwa bahili. Upepo unajitenga na mvua.
Na mto uliowahi kuimba bondeni unaanza kupungua—
kwanza kijito kidogo, kisha mawe yanaonekana, kisha udongo unapasuka.
Uhamisho haufiki wote kwa mara moja.
Unakuja kama msimu mrefu wa ukame—wiki kwa wiki, shamba kwa shamba.
Hii ni 2 Wafalme 24.

Katika siku zake akakwea Nebukadreza, mfalme wa Babeli na Yehoyakimu akawa mtumishi wake muda wa miaka mitatu; kisha , akageuka, akamwasi. 2 Naye Bwana akatuma juu yake vikosi vya Wakaldayo, na vikosi vya Washami, na vikosi vya Wamoabi, na vikosi vya wana wa Amoni, akawatuma juu ya Yuda ili kuiharibu, sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa mkono wa watumishi wake manabii....




Comments