Uchambuzi wa 1 Wafalme 10 — Malkia Langoni, Dhahabu kama Mvua, na Hekima Inayolifanya Mataifa Yakodoe Macho: Wakati Fahari Inapokuwa Jaribio la Kiroho
- Pr Enos Mwakalindile
- Feb 6
- 1 min read
Updated: Feb 19
Malkia anavuka majangwa akiwa na maswali.
Viungo vinasafiri juu ya ngamia.
Dhahabu inang’aa juani.
Na Yerusalemu—mji wa zaburi—
unakuwa jukwaa la hekima.
Mfalme anajibu.
Malkia anashusha pumzi.
“Ahimidiwe BWANA, Mungu wako...”
Kisha simulizi inaendelea kuhesabu.
Dhahabu kama mvua.
Pembe za tembo kama mifupa ya nchi.
Tausi kama rangi zilizomwagika duniani.
Na chini ya uso huo unaong’aa,
mtetemeko wa kimyakimya:
wakati utajiri unapozidi,
moyo utapenda nini zaidi?
Karibu katika 1 Wafalme 10.

Na malkia wa Sheba aliposikia habari za Sulemani juu ya jina la Bwana, alikuja ili amjaribu kwa maswali ya fumbo. 2 Akaingia Yerusalemu na wafuasi wengi sana, na ngamia wachukuao manukato, na dhahabu nyingi sana, na vito vya thamani; alipomfikilia Sulemani, akazungumza naye mambo yote aliyokuwa nayo moyoni....




Comments