Uchambuzi wa 1 Wafalme 21 — Shamba la Mizabibu Lililoibwa, Jina Lililosingiziwa, na Damu Iliyoahidiwa: Wakati Mamlaka Yanapommeza Jirani
- Pr Enos Mwakalindile
- 2 days ago
- 1 min read
Safari hii siyo vita vya majeshi.
Ni shamba la bustani.
Kiapo kidogo cha urithi,
udongo uliorithishwa kwa majina na sala.
Mfalme anakitamani.
Ananuna kama mtoto mchanga mwenye taji.
Malkia anaandika barua.
Wazee wanaitika kwa vichwa.
Mashahidi wa uongo wanasimama.
Mtu mwenye haki anaanguka.
Na damu inalowesha ardhi.
Kisha nabii anatokea
kama radi wakati wa adhuhuri:
“Je! Umeua, na kumiliki pia?”
Hapa ni 1 Wafalme 21.





Comments